VIDEO: SHUHUDIA EMMANUEL ADEBAYO AKISILIMU


 
Mshambuliaji wa kimataifa wa Togo Emmanuel Adebayor, miezi ya hivi karibuni amekuwa na akipitia kipindi kigumu katika klabu yake ya Tottenham Hotspur, huku pia akisakamwa na matatizo ya kifamilia kiasi cha kufikia hatua ya kuandika katika ukurasa wake wa Facebook .
Mwezi Mei mwaka huu, Tottenham walimpa muda wa mapumziko ili aweze kupata wasaa wa kusuluhisha matatizo yake ya kifamilia.
Huku mustakali wake na klabu yake ukiwa bado haujulikani, mshambuliaji huyo wa zamani wa Arsenal na Manchester City, leo ameamua kusilimu na kuwa Muislamu.
Katika video hapo chini Emmanuel Adebayor, Adebayor anaonekana akitoa shahada (akishahadia, ishara ya Kiislamu inayoashiria kumkubali Mungu na Muhammad kuwa ndiye Mtume wake), na kuthibitisha kuwa sasa amekuwa Muislamu rasmi.




Share on Google Plus

About mfaume

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment