IS WAUA RAIA 300 WA YAZIDI NCHINI IRAQ

Raia wa Yazidi waishio nchini Iraq.
KUNDI la wanamgambo wa Islamic State limewaua mateka takribani 300 ambao ni raia wa Yazidi kaskazini mwa Iraq.
Makamu wa rais nchini Iraq, Osama al-Nujifi ameyalaani mauaji hayo akiyataja kuwa ya kikatili.
Taarifa zimeeleza kuwa watu hao waliuawa katika wilaya moja iliyo magharibi mwa mji wa Mosul siku ya Ijumaa.
Wanamgambo wa Islamic State walithibiti maeneo yaliyo kaskazini mwa Iraq kwa karibu mwaka mmoja uliopita ambapo waliwaua na kuwashika mateka maelfu ya watu wa Yazidi wakiwaita makafiri.
Chanzo: BBC

Share on Google Plus

About mfaume

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment