HIVI NDIVYO MASHIA WALIVYOFANYA MAANDAMANO LEO

Imam wa Masjidi Ghadir, Hemed Jalala, akihutubia waumini (hawako pichani)
Baadhi ya waumini wakisikiliza jambo.Sehemu ya bango la maadhimisho hayo.
Picha za athari ya vita katika nchi mbalimbali. Sehemu ya waraka kwa Watanzania.
WAUMINI wa Madhehebu ya Shia wa msikiti wa Ghadiri uliopo Kigogo Post, jijini Dar es Salaam, leo wamefanya matembezi ya amani kuanzia Magomeni Mapipa mpaka viwanja vya Pipo vilivyopo Kigogo.
Akiwahutubia waumini walioshiriki maandamani hayo, Imam  wa msikiti huo, Hemed Jalala, amewataka waumini wa Kiislamu na wasio waislamu kudumisha amani ili kuepuka machafuko.
“Viongozi wa dini tuhimize waamini wetu katika kuliombea amani taifa letu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu,  Mungu ambariki kiongozi anayemaliza kipindi chake lakini pia atuongoze katika kumchagua kiongozi mwingine aliyekuwa bora na mwenye kupenda amani ili kuliepusha taifa na machafuko kama yanayozikumba nchi zingine za Kiarabuni ikiwemo Palestina,’’ alisema Jalala.


Share on Google Plus

About mfaume

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment