وَتَفَقَّدَ
الطَّيْرَ فَقَالَ مَا لِيَ لَا أَرَى الْهُدْهُدَ أَمْ كَانَ مِنَ
الْغَائِبِينَ ﴿٢٠﴾ لَأُعَذِّبَنَّهُ عَذَابًا شَدِيدًا أَوْ
لَأَذْبَحَنَّهُ أَوْ لَيَأْتِيَنِّي بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ ﴿٢١﴾ فَمَكَثَ
غَيْرَ بَعِيدٍ فَقَالَ أَحَطتُ بِمَا لَمْ تُحِطْ بِهِ وَجِئْتُكَ مِن
سَبَإٍ بِنَبَإٍ يَقِينٍ ﴿٢٢﴾ إِنِّي وَجَدتُّ امْرَأَةً تَمْلِكُهُمْ
وَأُوتِيَتْ مِن كُلِّ شَيْءٍ وَلَهَا عَرْشٌ عَظِيمٌ ﴿٢٣﴾ وَجَدتُّهَا
وَقَوْمَهَا يَسْجُدُونَ لِلشَّمْسِ مِن دُونِ اللَّـهِ وَزَيَّنَ لَهُمُ
الشَّيْطَانُ أَعْمَالَهُمْ فَصَدَّهُمْ عَنِ السَّبِيلِ فَهُمْ لَا
يَهْتَدُونَ ﴿٢٤﴾ أَلَّا يَسْجُدُوا لِلَّـهِ الَّذِي يُخْرِجُ الْخَبْءَ
فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَيَعْلَمُ مَا تُخْفُونَ وَمَا تُعْلِنُونَ
﴿٢٥﴾ اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ رَبُّ الْعَرْشِ الْعَظِيمِ ۩﴿٢٦﴾
(Sulaymaan)
Akakagua ndege, akasema: “Imekuwaje, mbona simuoni Al-Hud-hud, au
amekuwa miongoni mwa walioghibu? Bila shaka nitamuadhibu adhabu kali, au
nitamchinja, au aniletee hoja bayana (ya kughibu kwake).” Basi hakukaa
sana (mara alitokeza) akasema: “Nimegundua usilogundua na nimekujia
kutoka Sabaa na habari za yakini. Hakika mimi nimemkuta mwanamke
anawamiliki, na amepewa kila kitu, na anacho kiti cha enzi kikubwa.
Nimemkuta (yeye) na watu wake wanalisujudia jua badala ya Allaah, na
shaytwaan amewapambia ‘amali yao (hiyo), basi akawazuia na njia (ya
haki); kwa hiyo hawakuongoka. Hawamsujudii
Allaah Ambaye Anatoa yenye kufichika katika mbingu na ardhi na Anayajua
yale mnayoyaficha na yale mnayoyadhihirisha. Allaah - hakuna ilaaha (muabudiwa wa haki) ila Yeye, Rabb (Mola) wa Al-‘Arsh adhimu. [An-Naml: 20-26]
0 comments:
Post a Comment